IQNA-Wanaharakati wa kutetea haki za Wapalestina wamemsifu Meya wa Jiji la New York, Zohran Mamdani, kwa kufuta amri za kiutawala zilizokuwa zikizuia shughuli za makundi yanayounga mkono Palestina.
IQNA-Wanaharakati wa kutetea haki za Wapalestina wamemsifu Meya wa Jiji la New York, Zohran Mamdani, kwa kufuta amri za kiutawala zilizokuwa zikizuia shughuli za makundi yanayounga mkono Palestina.
IQNA – Harakati ya Ansarullah ya Yemen imetoa tamko kali kulaani shambulio la kijeshi lililofanywa na Marekani dhidi ya Venezuela, ikilitaja kuwa kitendo cha jinai.
IQNA – Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu amesisitiza kwamba kwa kumtegemea Mwenyezi Mungu na kusimama pamoja na wananchi “Inshaallah, tutampigisha magoti adui.”
IQNA – Imam Ali (AS) si mfano tu wa uchaji Mungu kama mtu binafsi na usafi wa moyo, bali pia ni kielelezo adimu cha uongozi wa haki, uwajibikaji na unaomweka mwanadamu katikati ya utawala, afisa mmoja wa Iraq amesema.
IQNA-Kampeni ya ‘Nadhiri ya Itikafu’, ambapo watu wanachangia kugharamia ibada ya Itikafu misikitini imezinduliwa nchini Iran. Itikafu ni kujitenga kwa ajili ya ibada, na nadhiri ni ahadi ya kidini na jukumu la hiari.
IQNA-Qari kutoka Iran ameshiriki katika usomaji Qur’an Tukufu katika hafla maalum iliyofanyika mjini Kakani, Bosnia na Herzegovina, usiku wa kuamkia Mwaka Mpya.
Amri ya hivi karibuni ya utawala wa Israel, iliyondoa mamlaka ya manispaa ya al-Khalil (Hebron) katika maamuzi ya mipango kuhusu eneo nyeti la msikiti huo, inaendelea kukosolewa vikali.
IQNA- Jamii ya Kiislamu Afrika Mashariki na hasa nchini Tanzania imekumbwa na msiba mkubwa kufuatia kufariki dunia kwa mwanazuoni mashuhuri, na mfasiri wa Qur'ani Tukufu, Sheikh Ali Jumaa Mayunga, aliyefariki dunia tarehe 1 Januari 2026, jijini Dar es Salaam, Tanzania.
IQNA-Rais Hassan Sheikh Mohamud wa Somalia amezinukuu ripoti za kiitelijinsia na kusema kuwa eneo lililojitenga la na nchi hiyo la Somaliland limekubali kuwapokea Wapalestina na kuanzishwa kambi ya kijeshi ya Israel katika eneo hilo mkabala wa kutambuliwa rasmi na Israel.
IQNA – Mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa linalohudumia wakimbizi wa Kipalestina ameonya kwamba vizuizi vipya vilivyowekwa na Israel vinakwamisha kabisa usambazaji wa misaada huko Gaza, vinazidisha hali ya njaa na kuweka “mfano hatari” kwa shughuli za kibinadamu duniani kote.
IQNA-Hatua ya kichokozi ya utawala wa Kizayuni wa Israel kutambua eneo la Somalia la 'Somaliland' kama nchi huuru kunahusishwa na mradi mpana zaidi wa kuchora upya ramani ya ushawishi katika Pembe ya Afrika na Bahari Nyekundu, mradi unaoendeshwa kwa misukumo ya kiusalama kwa ushirikiano wa utawala wa Israel na pia Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE).
IQNA – Katika hafla iliyovunja desturi za karne nyingi, Zohran Mamdani alianza rasmi muhula wake kama meya wa Jiji la New York siku ya Alhamisi kwa kuapa akiwa ameshika Qur’an Tukufu, tukio la kihistoria kwa Waislamu na kwa mandhari ya kisiasa ya jiji hilo kubwa.