IQNA

Ramadhani

Ujumbe wa Amani: Mtaa wa Frankfurt kupambwa kwa Taa za Ramadhani

15:45 - March 07, 2024
Habari ID: 3478463
IQNA - Barabara kuu ya kati huko Frankfurt, Ujerumani, itapambwa kwa taaza zenye nembo za hilali nyota na mapambo mengine kuadhimisha mwezi mtukufu wa Ramadhani.

Hatua hiyo ambayo ni ya kwanza kabisa mjini humo inalenga kutuma ujumbe wa amani na umoja wakati wa mwezi mtukufu wa Ramadhani, vyombo vya habari vya Ujerumani viliripoti.

Kuanzia Machi 12 hadi Aprili 11, mwezi wa kufunga na kutafakari kwa Waislamu, Grosse Bockenheimer Strasse njia ya wanaotembea kwa miguu wa Frankfurt – ambayo watu wa eneo hilo wanafahamu kama Fressgass (uchochoro wa chakula) kwa sababu ya kuenea kwa migahawa - itakuwa na maandishi makubwa yanayosomeka "Ramadhani Njema!" na mapambano mengine.

"Ramadhan ni wakati ambao watu hutafakari juu ya kile ambacho ni muhimu sana katika maisha: kuwa na kitu cha kula, paa juu ya kichwa chako, na amani na faraja na familia, marafiki na majirani," alielezea mwenyekiti wa baraza la jiji Hilime Arslaner.

"Nimefurahi kwamba jumbe hizi za amani wakati wa Ramadhani zitaonekana katika Frankfurt yetu," aliongeza.

Manispaa ya jiji hilo imetoa taarifa na kusema jumbe kama hizo ni muhimu hasa wakati wa vita na machafuko, na kuongeza: "Hizi ndizo mwanga wa umoja: dhidi ya chuki, ubaguzi, ubaguzi wa rangi dhidi ya Waislamu na pia chuki dhidi ya Wayahudi."

Ikiwa na wakazi wapatao 800,000, Frankfurt ni jiji la tano kwa ukubwa nchini Ujerumani (baada ya Berlin, Hamburg, Munich na Cologne) na kitovu cha sekta ya fedha nchini humo. Pia ni mojawapo ya miji ya Ujerumani yenye tamaduni nyingi huku Waislamu wakiwa karibu 15% ya wakazi (100,000-150,000).

Mohamed Seddadi, mwenyekiti wa Jumuiya ya Waislamu ya Frankfurt, kwa hiyo alikaribisha mipango ya kuupamba mji wakati wa Mwezi wa Ramadhani na kusema hatua hiyo ni "yenye maana sana kwa Waislamu," akisema inaashiria kwamba: "Sote ni pamoja."

Wakati taa za barabarani kwa muda mrefu zimekuwa sehemu ya sherehe za kidini za Kikristo, haswa wakati wa Krismasi, Waislamu katika nchi za Magharibi pia wameanza kupamba nyumba na majengo wakati wa Ramadhani, kulingana na Raida Chbib, mkuu wa Chuo cha Uislamu katika Utafiti na Jamii (AIWG) katika Chuo Kikuu cha Goethe huko Frankfurt.

3487460

Mipango ya Ramadhani ya Frankfurt kwa hiyo inakopa kutoka kwa vipengele vya utamaduni wa Kiislamu na Kikristo.

Habari zinazohusiana
captcha