Shirika la Huduma kwa jamii ya Qur'ani Tukufu, linalojulikana kama Huffaz, limechapisha tafsiri hiyo kama hatua ya kukabiliana na udhalilishaji wa Qur'ani Tukufu nchini Uswidi.
Abdul Aziz al-Rifa'ei, rais wa jamii, alisema tafsiri hiyo imetolewa kwa ushirikiano na Scandinavia Education Foundation.
Alisema ni tafsiri sahihi zaidi ya Qur’an Tukufu katika lugha ya Kiswidi
Pia inajumuisha tafsiri ya Kitabu Kitukufu kulingana na ufafanuzi maarufu wa Qur’ani, al-Rifa'ei aliongeza.
Pia alibainisha kwamba timu ya wasomi na watafsiri walishirikiana katika kuitafsiri tafsiri hiyo ya Aya za Qur’an Tukufu .
Al-Rifa'ei ameongeza kuwa jumuiya ya kutoa misaada inapanga kuchapisha na kusambaza maelfu ya nakala nyinginezo za tafsiri za Qur'ani Tukufu katika lugha tofauti.