IQNA

Sweden yamteua waziri wa kwanza Mwislamu

21:12 - October 12, 2014
Habari ID: 1459694
Mwanamke Mwislamu mwenye umri wa miaka 27 ameteuliwa kuwa waziri wa elimu nchini Sweden na hivyo kumfanya kuwa waziri wa kwanza Mwislamu katika nchi hiyo ya Ulaya.

Aida Hadzialic ambaye  ni Msweden mwenye asili ya Bosnia amehitimu kwa shahada ya sheria kutoka Chuo Kikuu cha Lundi na aliwahi kuwa naibu meya wa mji wa Halmstad nchini Sweden akiwa na umri wa miaka 23. Alizaliwamwaka 1987 huko Foča, Bosnia, na kuteuliwa huko kunamfanya mwanasiasa mwenye umri wa chini zaidi nchini Sweden kuwahi kuteuliwa kuwa waziri.
Hadzialic alikuwa na umri wa miaka mitano wakati familia yake ilipokimbia kutoka vita vya Bosnia-Herzegovina.
Ikumbukwe kuwa Bosnia ilitumbukia katika vita vya ndani mwaka 1992 ambapo watu laki mbili waliuawa na mamilioni ya wengine  kuachwa bila makao wakati vikosi vya Waserb vilipoanzisha mauaji ya kimbari dhidi ya Waislamu wa Bosnia.
Asilimia 15 ya raia wote wa Sweden walizaliwa katika nchi za kigeni. Inakadiriwa kuwa Waislamu ni karibu nusu milioni kati ya watu wote milioni tisa nchini humo.../mh

1459021

Kishikizo: sweden mwislamu aida
captcha