Kila mwaka na katika Ijumaa ya kwanza ya mwezi wa Muharram, kwa mnasaba wa kukumbuka alivyouawa shahidi kikatili Ali Asghar, mtoto mchanga wa miezi sita wa Imam Hussein (AS), Imam wa tatu wa Waislamu wa madhehebu ya Shia duniani, hufanyika kongamano na mjumuiko maalumu unaoshirikisha akina mama na watoto wao wachanga wanaonyonya.